Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) Yajadili Mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025
Mkuu wa Wilaya ya Pangani Mheshimiwa Zainab Abdallah, ameongoza kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC).
Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 24/02/2024 katika Ukumbi wa Zamani wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kwa ajili ya kujadili Mapendeke zo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2024/2025.
Awali akifungua kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Pangani Mh. Zainab Abdallah amesema kuwa kikao hiki ni kwa ajili ya kujadili mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti zetu kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025, hivyo tunapaswa kupitia vizuri bajeti zetu kwa maslahi mapana ya Wilaya yetu.
Afisa Mipango wa Wilaya Ndugu, Semion Vedastus aliwasilisha Mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri.
Ndg Vedastus amesema kuwa kwa Mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Wilaya ya Pangani inaomba kuidhinishiwa kukusanya na kutumia mapato yatokanayo na vyanzo vya ndani kiasi cha Shilingi19,552,457,000.00 ikiwa ni ongezeko la takriban 2% ya bajeti ya mwaka 2023/2024.
Kwa Upande wake Kaimu Meneja wa RUWASA Inj. Rajabu Yahya amesema kuwa Katika mpango wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2024/2025, Ruwasa, Wilaya ya Pangani imetengewa jumla ya Tsh. 2.499,960,304.10/= ambapo Fedha hizo zitawezesha kutekeleza jumla ya miradi 13, miradi 7 inaendelea na miradi 6 ni miradi mipya.
Vilevile Meneja wa TARURA Wilaya ya Pangani Inj. Mwita N Muhochi amesema kuwa katika mwaka wa Fedha 2024/2025 TARURA Wilaya ya Pangani inapendekeza kutumia jumla ya Tshs. 2,775,000,000 kwa matengenezo ya Barabara zenye jumla ya km 92.47 na makalvati 131.
Wajumbe mbalimbali wamempongeza Mwenyekiti wa kikao hicho na kuwaomba wataalam waendelee kupanga mipango na Bajeti zinazo akisi moja kwa moja uhalisia kwa maendeleo ya Wilaya ya Pangani.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa