Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani ndg Daudi Mwakabanje akiambatana na Afisa Ustawi wa Jamii ndg Kirigiti wameungana kutoa Elimu siku ya Maadhimisho ya Afya na Lishe.
Zoezi hilo limefanyika leo Tarehe 13 Februari, 2024, katika Kijiji cha Boza Wilayani Pangani ambapo Elimu mbalimbali kuhusu Lishe na Afya imetolewa.
Kwa upande wake Afisa Lishe Ndg Daudi Mwakabanje ameitaka jamii kuzingatia umuhimu wa Lishe bora ili kuondoa udumavu na utapiamlo katika jamii zetu.
"Jamii inapaswa kuelewa umuhimu wa kunyonyesha mtoto Maziwa ya Mama pekee ndani ya kipindi cha miezi sita ya mwanzo,".
Ameongeza pia ni muhimu kwa wakina mama kuhudhuria kliniki mapema mara baada wanapohisi ni wajawazito.
Aidha kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Ndg Kirigiti ametoa elimu juu ya Haki na Wajibu wa Watoto katika Jamii zetu ikiwa ni pamoja na kupata Elimu, Chakula na Maladhi.
Ameongeza kuwa ni muhimu kwa Wazee kuendelea kupatiwa Elimu juu ya Vitambulisho vya kuwatambua pamoja na namna sahihi ya kushughulikia migogoro ya kifamilia.
Mambo mengine yaliofanyika katika maadhimisho hayo ni pamoja na mapishi ya mfano, kufanya tathimini ya hali ya Lishe kwa watoto chini ya miaka mitano kwa kutumia (MUAC) pamoja na kupima uwiano wa uzito kwa Umri.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa