Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango imekipongeza kikundi cha mnufaika wa Mkopo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Pangani
Hayo yamefanyika leo Januari 18, 2024 wakati wa Ziara ya Kamati ya Fedha ilipomtembelea mnufaika huyo, Sokoni Pangani
Akiongea na Wajumbe wa Kamati hiyo, mnufaika wa mkopo huo ndugu Ramadhani Mzee amesema kuwa
"Kikundi cha ATHUMANI RAMADHANI MZEE kilifanikiwa kuomba mkopo wa Shilingi milioni tatu ( 3), kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Pangani chini ya Idara ya Maendeleo ya Jamii na kufanikiwa kupatiwa mkopo huo"
Mala baada ya kupokea fedha hizo kikundi kilinunua jumla ya Baiskeli 15 na kuanza kuzikodisha.
Ndg Mzee amesema anaishukuru Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan pamoja na Uongozi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, kwani hadi sasa Kikundi kimefanikiwa kurejesha Shilingi Milioni Moja na Nusu,na pia amefanikiwa kununua Viwanja na Kusomesha ndugu zake, kupitia mkopo huo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri mhe Akida Bahorera amempongeza ndg Athumani Mzee kwa mafanikio hayo makubwa na kuendelea kutoa wito kwa Vikundi vingine kuiga mfano bora na uzalendo kama wa kikundi cha ATHUMANI RAMADHANI MZEE.
Kikundi cha ATHUMANI RAMADHANI MZEE kinajihusisha na ukodishaji wa Baiskeli na kufanya shughuli zake maeneo ya Soko kuu la Pangani.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa