Pangani_ Tanga.
Kamati ya lishe Wilaya ya Pangani imefanya kikao cha utekelezaji wa Viashiria vy Mkataba wa Lishe Robo ya Nne Aprili hadi Juni kwa mwaka wa fedha 2023/2024 leo tarehe 24/07/2024, katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri (Mkoma) kikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Bw. Edward Charles Fussi.
Akiwasilisha taarifa ya Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Kaimu Afisa Lishe Wilaya Bw.Ibrahim Mohamed amesema kuwa
" katika robo ya nne divisheni ya lishe kimefanya tathmini ya hali ya lishe kwa wananchi kwa kutumia kipimo cha uwiano wa uzito kwa urefu(BMI), kufanya usimamizi shirikishi shuleni, kufanya Maadhimisho ya Siku ya afya na lishe katika vijiji(SALiKi) pamoja na kushiriki katika utoaji wa huduma wa afya mseto( afya gulio)". Alisema.
Aidha kwa upande wake mkuu wa Divisheni ya elimu ya awali na msingi ndg Juma Mbwela amebainisha changamoto zinazoikabili idara hiyo ikiwa ni pamoja na uchangiaji duni wa wazazi hali inayopelekea wanafunzi wengi kupata uji badala ya chakula cha mchana.
Ndugu Juma Mbwela amesisitiza kuwa idara kwa kushirikiana na Afisa Lishe wanaendelea na hamasa kupitia vikao vya Uwawa, na kuhamasisha wadau ili kusaidia upatikanaji wa majiko ya kupikia. Aliongeza.
Kwa upande wake mkuu wa idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu bi Veronica Marwa amesisitiza kuwa agenda ya lishe izidi kupewa kipaumbele katika jamii zetu.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa