Kambi ya Watalaamu wa Afya kutoka Uturuki iliyodumu kwa muda wa siku 6 wilayani Pangani imehitimishwa ,kambi hiyo imehusisha utoaji wa huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na upimaji wa Magonjwa ya Macho na kutoa Tiba.
Zoezi hilo la Upimaji wa Magonjwa ya Macho limehitimishwa leo Septemba 21,2023 katika Hospitali ya Wilaya ya Pangani.
Lengo kuu la Wataalamu hao wa Afya lilikuwa ni Kufanya uchunguzi wa matatizo ya macho , kufanya upasuaji wa mtoto wa jicho, kutoa dawa pamoja na kutoa miwani, kwa wagonjwa waliobainika.
Hafla hiyo ya kufunga imehudhuriwa na Katibu tawala wa Wilaya ya Pangani Ndugu, Ester Gama, pamoja na Katibu wa Mbunge.,Ambapo wote kwa pamoja walitoa neno la shukrani kwa Wataalamu hao na kuwakaribisha tena kurudi kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wa Pangani
Zoezi hilo la siku 6 limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani zaidi ya Wananchi 1,000 walifikiwa na kupatiwa huduma stahiki bila malipo yoyote.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa