Zoezi la ukarabati wa majengo mbalimbali ya Hospitali kongwe ya Wilaya ya Pangani unaendelea na umefikia hatua nzuri.
Ameyasema hayo Katibu wa Afya wa Wilaya ya Pangani, Ndugu Bruno Mlay, na kupongeza jitihada hizo zinazofanywa na serikali katika ukarabati huo.
Ukarabati huu umetokana na ruzuku kutoka serikalini ya jumla ya fedha milioni mia tisa (900M), ambazo zimetolewa na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa,Dkt Samia Suluhu Hassan, na kuwezesha ukarabati huo kwenda vizuri.
Aidha wakazi wa Pangani wamempongeza Rais kwa kukarabati Hospitali hiyo kongwe ya wilaya na kusema kuwa " Tunamshukuru Mheshimiwa Raisi mama yetu kwani hospitali hii ni msaada mkubwa kwetu na ukarabati huu unatuwezesha kupata huduma salama na kwa urahisi;
Hata hivyo zoezi la ukarabati wa Hospitali hii kongwe ya Wilaya ya Pangani bado unaendelea na upo katika hatua nzuri.
#panganidc
#kazi iendelee
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa