Mh. Zainab Abdallah ameendelea na ziara yake ya twende na samia kijiji kwa kijiji nakusiikiliza kero mbali mbali za wananchi.
Akiwa katika kijiji cha Mkalamo Wilayani Pangani tarehe 10.07.2023, amezungumza na kikundi cha kina mama cha Mapambano group.
Kiongozi wa Kikundi hicho amesema kuwa"kikundi cha Mapambano group tunaishukuru halmashauri ya wilaya ya Pangani kwa mkopo wa shilingi milioni 5,158,000, waliotupa mwaka 2021, mkopo huo umetubadirishia maisha na mpaka sasa tupo kwenye hatua nzuri za marejesho".
Afisa maendeleo ya jamii Wilaya Bi. Sekela Mwalukasa amewapongeza wanakikundi hao na kusema kuwa "kikundi hiki kinafanya vizuri sana kurejesha mkopo wao kwa wakati".
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Pangani ameungana na Mhe. Mbunge wa Pangani Juma Aweso na kutoa jumla ya shilingi milioni moja kuunga mkono juhudi za kikundi hicho, na kutoa wito kwa wananchi kujisajiri na kujiunga na vikundi mbali mbali kwa maendeleo ya wanapangani.
Mapambano group ni kukundi kilichojikita kwenye biashara ya uuzaji wa chakula na wameeleza mafanikio ya mkopo huo ikiwa ni pamoja na kumiliki viwanja na kusomesha watoto wao.
#twendenasamia
#kijijkwakijiji
#panganimpya
#kaziiendelee
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa