Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga cde Rajab Abdurrahman Pamoja na Mbunge wa Jimbo la Pangani ambae pia ni Waziri wa Maji mhe Jumaa Aweso wamechangia ujenzi wa Zahanati katika Kijiji cha Mwembeni kilichopo Wilayani Pangani
Hayo yamefanyika wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa mkoa wa Tanga kukagua miradi ya maendeleo ambapo Mwenyekiti wa CCm mkoa wa Tanga amechangia jumla ya Shilingi Milioni 10 kwaajili ya ujenzi wa Zahanati hiyo.
Akipokea fedha hizo Mkuu wa Wilaya ya Pangani mhe Zainab Abdallah amesema kuwa
" kipekee naishukuru kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga chini ya Mwenyekiti wake Cde Rajab Abdurrahman kwa kuchangia fedha hizi kwaajili ya ujenzi wa Zahanati hii, lakini pia namshukuru mbunge wa jimbo la Pangani ambae pia ni Waziri wa Maji mhe Jumaa Aweso kwa kuchangia jumla ya tofali elfu mbili (2 ) pamoja na mifuko 100 ya saruji,ili kuhakikisha Zahanati hiyo inajengwa.
Aidha amewapongeza viongozi wote kwa kuunga mkono juhudi za uchangiaji wa ujenzi wa Zahanati hiyo na kuahidi kuwa Serikali itasimamia ujenzi huo na kuhakikisha unakamilika kwa ubora uliokusudiwa ili kuweza kutoa huduma kwa wananchi.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa