• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Pangani District Council
Pangani District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Fedha Uchumi na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • kilimo Umwagiliaji na ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya jamii na vijana
      • Ujenzi
      • Enviroment and Sanitation
    • vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Beekeeping
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uvuvi na Hifadhi ya Bahari
    • Biashara na Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Huduma za kijamii
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmshauri
      • Kamati ya fedha ,mipango na uongozi
      • Kamati ya Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya uchumi ujenzi na mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Repoti Mbalimbali
    • Mwongozo
    • fomu mbalimbali
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa umma
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YATOA MWEZI MMOJA KWA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE 2024 KUBADILISHA MACHAGUO YA TAHASUSI ZA KIDATO CHA TANO.

siku ya kuwekwa : April 2nd, 2025

SERIKALI kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI inatoa fursa ya mwezi mmoja kwa wanafunzi waliohitimu Kidato cha Nne mwaka 2024 kubadili tahasusi au kozi itakayomwandaa kuwa na utaalamu stahiki katika maisha yao ya baadaye.


Utaratibu huo umeanza Machi 31 hadi Aprili 30 mwaka huu.


Akizungumza na waandishi wa Habari leo tarehe 02.04.2025 jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa alisema hatua hiyo inatoa fursa kwa wanafunzi kubadilisha machaguo ya Tahasusi za Kidato cha Tano na Vyuo vya Kati na Elimu ya Ufundi kwenye mfumo wa kielektroniki wa uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na Kidato cha Tano na Vyuo.


“Hatua hii ni maandalizi ya awali ya uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga Kidato cha Tano na Vyuo vya Serikali kwa mwaka 2025.”

Serikali imekuwa ikitoa fursa kwa wahitimu wa Kidato cha Nne kufanya mabadiliko ya machaguo ya Tahasusi (combination) na Kozi mbalimbali walizozichagua kupitia Fomu ya Uchaguzi (Selform.).


Fursa hii huwawezesha wanafunzi kurekebisha machaguo yao kulingana na ufaulu waliopata kwenye matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).


Mchengerwa alisema Serikali kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI imekamilisha utaratibu wa awali wa kuingiza kwenye kanzidata taarifa zilizo kwenye fomu za uchaguzi za wanafunzi kama zilivyojazwa na wanafunzi wakiwa shuleni.


“Baada ya wanafunzi kufanya marekebisho yao, kanzidata hiyo ndiyo itakayotumika kuwachagua na kuwapangia nafasi za Kidato cha Tano na Kozi mbalimbali katika Vyuo vya Kati na vya Elimu ya Ufundi kwa kuzingatia sifa za ufaulu na machaguo yao.”


“Ofisi ya Rais – TAMISEMI inatoa fursa kwa wahitimu wa elimu ya sekondari Kidato cha Nne, mwaka 2024 kubadili machaguo yao ili kutoa nafasi zaidi kwa mwanafunzi kusoma tahasusi au kozi itakayomwandaa kuwa na utaalamu stahiki katika maisha yake ya baadaye.”


Mhe. Mchengerwa alisema hatua hiyo pia itatoa fursa zaidi ya wanafunzi kuongeza machaguo na kufanya machaguo mapya ya Tahasusi na Kozi.


“Napenda kuwasihi wazazi na walezi kushauriana kikamilifu na watoto wao na kupata ushauri wa kitaalamu na kabla ya kufanya machaguo sahihi ya tahasusi na kozi kulingana na ufaulu wao.”


Wanafunzi, wazazi na walezi wanakumbushwa kushauriana kikamilifu ikiwa ni pamoja na kupata ushauri wa kitaalam na kitaaluma kabla ya kufanya mabadiliko ya tahasusi au Kozi.


Mchengerwa amewahimiza wahitimu wote wanahimizwa kufanya marekebisho ya machaguo ya tahasusi na kozi kulingana na ufaulu wao, kwa kuingia kwenye Mfumo wa Uchaguzi wa Wanafunzi unaopatikana kupitia kiunganishi cha selform.tamisemi.go.tz.


Akielekeza namna ya wahitimu kuingia kwenye mfumo, Mchengerwa alisema mhitimu anapaswa kuandika jina lake la mwisho, mwaka wa kuzaliwa na alama za ufaulu alioupata kwenye somo atakaloulizwa na mfumo au swali lolote atakaloulizwa.


“Ni matumaini yangu kuwa wahitimu wote watatumia kwa ukamilifu fursa waliyopewa ya kubadilisha tahasusi na kozi kulingana na ufaulu waliopata. Pia wataweza kusoma tahasusi au kozi ambazo wamefaulu vizuri ama wana malengo nazo zaidi.”


Mhe. Mchengerwa alisema baada ya kukamilika kwa utaratibu huo na wanafunzi kupangiwa shule na vyuo, hakutakuwa na fursa ya wazazi na wanafunzi kubadili tahasusi na kozi zao.


“Ninawasisitiza wanafunzi, wazazi na walezi kutumia muda huo vyema ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza mara baada ya matokeo ya uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo kutangazwa.”


“Baada ya matokeo ya kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo kutangazwa, Ofisi haitashughulikhuduma ya kubadilisha tahasusi na zoezi hili ni bure.”

Tangazo

  • MPYA: TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA PANGANI May 10, 2023
  • MPYA: TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • MPYA: ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO September 09, 2023
  • MPYA: ORODHA YA WATAKAOENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO September 09, 2023
  • Angalia zote

Habari za Sasa

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI.

    May 23, 2025
  • WILAYA YA PANGANI YAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE – ROBO YA TATU 2024/2025.

    May 19, 2025
  • RC BATILDA AIPONGEZA PANGANI UANDIKISHAJI WA DAFTARI AWAMU YA KWANZA NA KUTOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA AWAMU YA PILI

    May 16, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI NA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI LAANZA PANGANI

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

ujenzi wa barabara ya Tanga pangani
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Mwongozo wa Tehama
  • Ratiba ya Vikao vya Halmashauri
  • Miongozo mbalimbali

Kurasa za mfanano

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Miongozo mbali mbali
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Pangani District Council

    Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga

    Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058

    Namba ya simu: 0658100588/062289307

    Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz

Mawasiliano Mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa