Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu (2 in 1) Wafikia Hatua Nzuri - Kata ya Mkalamo, Wilaya ya Pangani
Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza kwa vitendo dhamira ya kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wa umma
Katika Kata ya Mkalamo, ujenzi wa nyumba ya walimu ya aina ya 2-in-1 umefikia hatua nzuri sana, ukifadhiliwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu.
Mradi huu ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha walimu wetu wanapata makazi bora na ya karibu na maeneo yao ya kazi, ili kuongeza ufanisi na motisha kazini.
Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuweka kipaumbele kwenye sekta ya elimu na ustawi wa watumishi wake.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa