Mkuu wa Wilaya ya Pangani Mheshimiwa Zainab Abdallah amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga mhe Waziri Kindamba katika uzinduzi rasmi wa Mradi wa Ardhi Mkoani Tanga, uliofadhiliwa na European Union pamoja na World Vision Ireland.
Mradi huu wenye Thamani ya Shilingi Bilioni 6 unatarajiwa kutekelezwa kwenye Wilaya ya Pangani,Handeni,Mkinga pamoja na Kilindi, Mkoani Tanga.
Aidha mradi huu unalenga kuwagusa Wanawake na Vijana na unakusudia kukabiliana na mabadiliko ya Tabia nchi kwa kuhifadhi mazingira na utunzaji wa misitu ikiwa ni pamoja na kutumia nishati mbadala ya kupikia badala ya matumizi ya Mkaa.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani ndg Juma Mbwela ameshiriki uzinduzi huo.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa