Halmashauri ya Wilaya ya Pangani leo Januari 19,2024,imezindua program Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto, katika ukumbi wa Halmashauri.
Akifungua kikao hicho cha Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani ndg Veronica Marwa amewakaribisha wawezeshaji na kuwataka Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Lishe pamoja na maafisa Ustawi Jamii walioshiriki kuwa maborozi wazuri katika Jamii juu ya utekelezaji wa program hii.
"Wataalamu wenzangu nichukue fursa hii kuwakumbusha kuwa program hii ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto imeshazinduliwa katika ngazi ya Kitaifa,kimkoa na sasa ni zamu ya Wilaya, na sisi tuko tayari kuipokea rasmi na kuanza utekelezaji".
Akiwasilisha mada ya Sayansi ya Makuzi na Maendeleo ya Awali kwa mtoto ndug Regis Temba Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la UHTC amesema kuwa -:
"Programu hii inalenga kutoa huduma Jumuishi kwa Watoto katika maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na afya bora, lishe, ujifunzaji wa awali, malezi ya mwitikio, pamoja na ulinzi na usalama kwa watoto wenye umri wa miaka sifuri hadi nane (0-8)."
Kwa upande wake ndg Mmasa amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuwekeza ipasavyo katika eneo la Lishe, Afya, malezi yenye mwitikio, pamoja na Kuimarisha ushirikiano na wadau wote.
"Muongozo huu una sura tisa ambazo zinahusisha mikataba ya Kitaifa na Kimataifa pamoja na Matokeo yanayotarajiwa katika kutekeleza mkakati huu muhimu,Gharama, Utawala na Usimamizi.
Programu hii ni juhudi muhimu za kuimarisha huduma za kijamii kwa watoto katika Wilaya ya Pangani na inalenga kuhakikisha kuwa watoto wanapata fursa bora za makuzi na malezi, pamoja na ulinzi dhidi ya hatari zozote zinazoweza kuwakabili.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa