• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Pangani District Council
Pangani District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Fedha Uchumi na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • kilimo Umwagiliaji na ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya jamii na vijana
      • Ujenzi
      • Enviroment and Sanitation
    • vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Beekeeping
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uvuvi na Hifadhi ya Bahari
    • Biashara na Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Huduma za kijamii
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmshauri
      • Kamati ya fedha ,mipango na uongozi
      • Kamati ya Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya uchumi ujenzi na mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Repoti Mbalimbali
    • Mwongozo
    • fomu mbalimbali
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa umma
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya Picha

Uvuvi

 UTANGULIZI

Wilaya iinatekeleza shughuli zote za Uvuvi kama ilivyo ada, shughuli hizo ni pamoja na kusimsmia sheria, kanuni na sera za uvuvi ili kuhakikisha kunakuwepo na ulinzi,uhifadhi,utunzaji na uvunaji endelevuwa rasilimali za uvuvi pamoja na utunzaji wa mazingira yake,lengo kuu ni kuhakikisha rasilimali ya uvuvi inatumiwa na kizazi cha sasa na cha baadae kwa maendeleo ya jamii na wilaya kwa ujumla.

HALI YA UVUVI

Hali ya uvuvi katika wilaya yetu ya pangani ni ya wastani pamoja na changamoto mbalimbali zilizopo za uvuvi haramu zana duni na vyombo duni kwa wavuvi wengi wa pangani lakini shughuli za uvuvi zimeendelea kufanyika hadi kufikia robo ya pili ya mwaka2016/2017 jumla ya kilo 38,525 zenye thamani ya tshs 154,100,000/= zilivunwa.

 

HUDUMA ZA UGANI

Huduma za ugani  zinazotolewa ni pamoja na ufugaji samaki, ukulima wa mwani,uvuvi unaozingatia uhifadhi wa  mazingira pamoja na uundaji wa vikundi  vya usimamizi shirikishi wa rasilimali za uvuvi yaani Beach Management Unit(BMUs) na kuvijengea uwezo wa kufanya kazi ikiwa ni pamoja na mafunzo.

IDADI YA WAVUVI NA VYOMBO

Kwa mujibu wa sense ya uvuvi iliyofanyika mwezi wa pili mwaka 2016 Wilaya ya Pangani ina jumla ya wavuvi1540 wanaojishughulisha na uvuvi wa samaki, pweza kamba na kaa na wavuvi 62 wanaojighulisha na utandaji wa uduvi ambao kwa mujibu wa sheria ya uvuvi no.22 ya mwaka 2003.

Mchanganuo   vyombo 271 vya uvuvi  

s/n
Aina ya chombo
Idadi
1
Ngalawa
196
2
Madau
2
3
Boti
9
4
Mashua
13
5
Mitumbwi
51

Jumla
271


MAFANIKIO

Kitengo cha uvuvi kwa  kushirikiana na mamlaka ya chuo cha ufundi stadi VETA kwa awamu tofauti tulifanikiwa kutoa elimu kwa wavuvi sitini (60) juu ya ujasiriamali, uchakataji na usindikaji wa samaki, VVU na Ukimwi kwa wadau wa uvuvi wa vijiji vya Ushongo, Stahabu, Pangani mashariki na Pangani magharibi na (wavuvi kumi na tano kwa kila kijiji) kuweza kutunukiwa vyeti kwa wavuvi  hao. Sambamba na mtaalamu mmoja wa uvuvi aliefanikiwa kwenda kujiendeleza kwa ngazi ya shahada.

Mbali na wavuvi hao kupata elimu bado wavuvi wameendelea kupata kipato kutoka katika sekta ya uvuvi kwa kujishughulisha na shughuli mbalimbali za uvuvi na  kufanikiwa kuvuna tani 65,079 zenye thamani ya Tshs 182,316,000 /= kwa mwaka 2015/2016 ukilinganisha na tani 52,506 zenye thamani ya Tshs 151,105,880/= waliovunwa kwa mwaka 2014/2015.

Kitengo cha uvuvi kimefanikiwa katika suala zima la ukusanyaji maduhuri ambapo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 kitengo cha uvuvi kiklipangiwa kukusanya Tshs 32,598,400/= na kuweza kuvuka lengo kwa kukusanya Tshs 35,517290/= sawa na asilimia miamoja ishirini na moja (121%) ukilinganisha na mwaka 2014/2015 ambapo lengo lilikua Tshs 27,598,400/= na kufanikiwa kukusanya Tshs 23,889,650/= sawa na asilimia sabini na tatu(73%)

 

AINA YA SAMAKI WANAOPATIKANA PANGANI.


CHANGAMOTO

Kumekuwa na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta uvuvi katika wilaya Pangani changamoto hizo zimegawanywa kwa makundi yafuatayo:-

Kwa wavuvi- Changamoto kubwa walionayo  wavuvi wa pangani ni zana na vyombo vyao kuwa duni hivyo kupelekea wavuvi wengi kufanya uvuvi mdogo na unaogharimu muda mwingi na mavuvi kidogo hivyo kupelekea kuwa na kipato kidogo.

Uvuvi haramu  

Uvuvi haramu bado ni changamoto mbali na kitenggo cha uvuvi kujitahidi kufanya doria za mara kwa mara .

 

Kitengo cha uvuvi kimefanya jumla ya doria tisa (9) kuanzia mwaka 2015 mpaka sasa na kufanikiwa kukamata zana haramu ambazo ni kokoro/juya ishirini na moja(21),Nyavu za timba(monofilament) kumi na tano(15).Nyavu za makila zenye matundu madogo(gillnet) tano (5),Vimia (castnet) kumi na tano(15) na mikuki/michinji ishirini na sita (26) na kamba zenye urefu wa mita 9,400.

 

Sambamba na doria hiyo watuhumiwa ishirini na nne(24) walikamatwa na kupigwa faini na wengine wawili(2) kufikishwa polisi kutokana na uzito wa makosa yao na kufunguliwa kesi  zenye jalada DOGORI NA SUFIANI - PAN/218/2017 (uvuvi wa sumu eneo la Mkwaja) wavuvi wengine walikimbia na kutelekeza pikipiki mbili ambazo zipo kituo cha polisi huku wakitafutwa kwa hati ya kukamata namba PAN/RB/36/2017 na PAN/RB/163/2017

 

Changamoto ya ukosefu wa Ruzuku ya uendeshaji wa ofisi (OC)

Kitengo cha uvuvi kimekua na changamoto nyingi ya uwezeshwaji ili kutekeleza majukumu yake ambapo imekukuwa ikitegemea mapato ya ndani kwa kuwa haipati ruzuku kutoka serikali kuu. Pamoja na kuchangia mapato mengi katika Halmashauri  kitengo cha uvuvi hakirejeshewi asilimia 15 ya makusanyo kama ilivyoelekezwa na Ofisi ya Rais Tamisemi kutokana na Halmashauri kuwa na vyanzo vichache vya mapato ambavyo havikidhi mahitaji ya fedha ya Halmashauri

Ukosefu wa Vitendea kazi

Aidha kitengo cha uvuvi kimekuwa na uhaba wa vitendea kazi kama vile boti ya doria kwa ajili ya kufanya doria za majini, kwa sasa Boti ndogo iliyoletwa chini ya Mradi wa MACEMP ndiyo inayosaidia doria ndogondogo kutokana na kuwa na uwezo mdogo wa kufanya doria

1 MATARAJIO NA UTATUZI WA CHANGAMOTO

Matarajio ya kitengo cha uvuvi ni kuendelea kupambana na kuhakikisha tunadhibiti utoroshaji wa mazao ya uvuvi ili kuweza kufikia lengo la kukusanya Tsh 150,000,000/= ambapo hadi kufikia tarehe ishirini ya mwezi wa pili (28/02/2017) tulikua tumeshakusanya Tshs 75,000,000/= ni matarajio yetu kuwa ikiwa asilimia 15 ya makusanyo haya yatarudishwa kwenye kulinda kutunza na kuhifadhi rasilimali ya uvuvi tutafikia lengo la kuongeza mazao ya uvuvi kufikia tani 80,000 kwa mwaka.

 

Kuendelea kutoa elimu ya ugani kwa wavuvi  juu ya uvuvi endelevu na wenye tija, kwa wafanyabiashara ya samaki juu ya njia bora na salama za uhifadhi samaki na elimu ya ufugaji samaki ili kuweza kujiongezea kipato na kuinua uchumi.

Kitengo cha uvuvi kinaendelea kufanya doria za mara kwa mara ili kupambana na uvuvi haramu na utoroshaji wa mazao ya uvuvi

Wilaya ya Pangani ni mojawapo ya wilaya zilizochaguliwa kuwa za mfano kutekeleza mradi wa SWIOFish ambapo kitengo cha uvuvi kinatarajia  kuimarisha usimamizi wa rasilimali za uvuvi kwa kushirikisha jamii katika kulinda, kutunza, kuhifadhi rasilimali za bahari pia kusimamia sera, sheria na kanuni za uvuvi ili kuwa na uvuvi endelevu kwa manufaa ya jamii na wilaya kwa ujumla.

Kitengo cha uvuvi kinatarajia kutekeleza vipengele vyote vya mradi kikishirikiana na jamii ya wavuvi ili kudumisha usimamizi unaozingatia ekolojia ya mazingia.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA KUKUSANYA TAARIFA ZA ANWANI YA MAKAZI NA POSTIKODI HALMASHAURI YA PANGANI April 10, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA KAZI YA AFISA MTENDAJI WA KIJIJI NA DREVA March 16, 2022
  • MAUZO YA VIWANJA June 04, 2018
  • VIBALI VYA UJENZI August 15, 2018
  • Angalia zote

Habari za Sasa

  • MAAFISA WATENDAJI KATA 6 PANGANI DC, WAPATA MGAO WA PIKIPIKI ZA SERIKALI AWAMU YA KWANZA

    February 17, 2023
  • WALIMU WA SHULE ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA PANGANI WAISHUKURU SERIKALI KWA KUWAGAWIA VISHIKWAMBI KWAAJILI YA KUFUNDISHIA

    January 12, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2022

    January 04, 2023
  • WILAYA YA PANGANI YAPOKEA ZAWADI ZA CHRISTMAS NA MWAKA MPYA 2023 KUTOKA KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH, DR. SAMIA SULUHU HASSAN.

    December 24, 2022
  • Angalia zote

Video

ujenzi wa barabara ya Tanga pangani
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Mwongozo wa Tehama
  • Ratiba ya Vikao vya Halmashauri
  • Miongozo mbalimbali

Kurasa za mfanano

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Miongozo mbali mbali
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Pangani District Council

    Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga

    Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058

    Namba ya simu: 0658100588/062289307

    Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz

Mawasiliano Mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa