• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Pangani District Council
Pangani District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Fedha Uchumi na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • kilimo Umwagiliaji na ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya jamii na vijana
      • Ujenzi
      • Enviroment and Sanitation
    • vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Beekeeping
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uvuvi na Hifadhi ya Bahari
    • Biashara na Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Huduma za kijamii
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmshauri
      • Kamati ya fedha ,mipango na uongozi
      • Kamati ya Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya uchumi ujenzi na mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Repoti Mbalimbali
    • Mwongozo
    • fomu mbalimbali
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa umma
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya Picha

Maji

Mamlaka ya Maji Mjini inahudumia Mji wa Pangani pamoja na Vijiji vinavyouzunguka Mji huu. Jumla ya wakazi wapatao 14,423 walilengwa kupata kupata huduma ya Maji safi  kutoka katika Visima Virefu (BH) 4 vilivyoko katika Kijiji cha Boza. Hata hivyo, idadi ya watu wanaopata Maji ni 8,076 ambao ni sawa na asilimia 56 (56%) ya walengwa wote.

Lakini kutokana na kuharibika mara kwa mara kwa mitambo chakavu ya kusukuma maji, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa muda mwingi inakadiriwa kuwa chini ya asilimia 45 ya mahitaji .

Pamoja na matatizo mengine, Mradi wa Maji Mjini unakabiliwa na changamoto kuu zifuatazo;

a)Tofauti kubwa iliopo baina ya utashi na ugavi

(Demand and Supply), uzalishaji wa Maji ni mita za ujazo 900 kwa siku wakati mahitaji ya Maji ni mita za ujazo 1,600 kwa siku sawa na asilimia 56 (56%).

b) Miundombinu ya kusambaza Maji na Mitambo chakavu;  Miundombinu ya kusambaza Maji imejengwa kwenye miaka ya 1960s na kwa sasa imechakaa sana na huathiri utoaji wa huduma kwa kiasi kikubwa

c) Katizo la umeme la mara kwa mara; kutokana na kutokuwepo kwa ‘’standby Generator’’, kiwango cha uzalishaji Maji hupungua sana.

d) Kiwango kikubwa cha upotevu wa maji (non revenue water) kutokana na wateja wengi kutokuwa na dira za maji.

Ili kukabiliana na changamoto zilizoainishwa hapo juu, Wizara ya Maji ilimwajiri Mtaalamu Mshauri (ARAB CONSULTING ENGINEERS) kufanya upembuzi yakinifu ( Feasibility studies) mwaka 2009.

Mtaalamu Mshauri  alitoa mapendekezo yafuatayo:-

a) Ufumbuzi wa muda mfupi (Short term solution) kuongeza uzalishaji Maji kwa kuchimba Visima virefu 3 na kuboresha Miundombinu ya kusambaza Maji kwa makadirio ya gharama Tsh. 747,000,000/= (2009).

b) Ufumbuzi wa muda mrefu (Long term solution) unalenga kuchukua maji kutoka mto Pangani na makadirio ya gharama za utekelezaji ni Tsh Bilioni.10.6 (2009).

UKARABATI WA MRADI WA MAJI MJINI.

Kupitia maombi maalum (Other Grants) 2014/2015 Halmashauri ya Wilaya ilipokea kiasi cha Tsh 200,000,000 kati ya Tsh 400,000,000 zilizoombwa kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya mradi wa maji Mjini awamu ya kwanza. Kwa sasa ukarabati wa miundombinu ya usambazaji maji awamu ya kwanza umekamilika. Hatua hii imesaidia kuongeza kiwango cha uzalishaji wa Maji na kuwa mita za ujazo 900 kwa siku kutoka mita za ujazo 700 kwa siku.

Katika bajeti ya mwaka 2015/16, kwa upande wa maji mjini tuliidhinishiwa Tshs 200 milioni kupitia maombi maalum (Other Grants) lakini hatukupokea fedha hizo.

Mwezi Oktoba 2016 tumepokea Tshs 200 milioni kutoka Wizara ya maji kwa ajili ya kuendeleza ukarabati wa miundo mbinu ya kusambaza maji mjini awamu ya II na kuweka mfumo wa kielektroniki wa  ukusanyaji mapato . Hata hivyo ni muhimu kwa fedha kuendelea kupatikana ili ukarabati uweze kufanyika awamu kwa awamu.

MAJI VIJIJINI

Malengo ni kuona kuwa  upatikanaji wa maji katika umbali usiozidi mita 400 kutoka makazi ya wananchi. Kupitia Programu ya Maji na Usafi na Mazingira Vijijini (NRWSSP), Ujenzi wa miradi ya Maji katika vijiji nane vya Madanga, Jaira, Bweni, Kwakibuyu, Kigurusimba, Mzambarauni, Boza na Madanga  imekamilika. 

Wakazi wa Vijijini wapatao 29,560 hupata huduma ya maji safi karibu na makazi yao ambapo ni sawa na 66% ya wakazi wote 44,788 wa Vijijini.

Tangazo

  • MPYA: TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA PANGANI May 10, 2023
  • MPYA: TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • MPYA: ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO September 09, 2023
  • MPYA: ORODHA YA WATAKAOENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO September 09, 2023
  • Angalia zote

Habari za Sasa

  • WILAYA YA PANGANI YAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE – ROBO YA TATU 2024/2025.

    May 19, 2025
  • RC BATILDA AIPONGEZA PANGANI UANDIKISHAJI WA DAFTARI AWAMU YA KWANZA NA KUTOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA AWAMU YA PILI

    May 16, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI NA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI LAANZA PANGANI

    May 16, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • Angalia zote

Video

ujenzi wa barabara ya Tanga pangani
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Mwongozo wa Tehama
  • Ratiba ya Vikao vya Halmashauri
  • Miongozo mbalimbali

Kurasa za mfanano

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Miongozo mbali mbali
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Pangani District Council

    Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga

    Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058

    Namba ya simu: 0658100588/062289307

    Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz

Mawasiliano Mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa