• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Pangani District Council
Pangani District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Fedha Uchumi na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • kilimo Umwagiliaji na ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya jamii na vijana
      • Ujenzi
      • Enviroment and Sanitation
    • vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Teknolojia Habari na Mawasiliano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Beekeeping
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uvuvi na Hifadhi ya Bahari
    • Biashara na Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Huduma za kijamii
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmshauri
      • Kamati ya fedha ,mipango na uongozi
      • Kamati ya Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya uchumi ujenzi na mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Repoti Mbalimbali
    • Mwongozo
    • fomu mbalimbali
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa umma
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya Picha

DC MUSSA KILAKALA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE ROBO YA TATU(JANUARI HADI MACHI 2024).

siku ya kuwekwa : May 18th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Pangani mhe Mussa Kilakala leo tarehe 18 Mei, 2024 ameongoza kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe katika ukumbi wa zamani wa Halmashauri.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya Lishe kwa kipindi cha robo ya Tatu, Afisa Lishe Wilaya ndg Daudi Mwakabanje amesema kuwa,


" Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kupitia Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe imekua  ikitekeleza afua mbalimbali za Lishe kwa kufuata mwongozo wa Taifa wa Lishe na kutoa Elimu na unasihi wa Lishe, kushiriki katika ufunguzi wa program jumuishi ya Taifa  (PJT_MMMAM) katika ngazi ya Halmashauri, kufanya Maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe katika vijiji 33, kufanya usimamizi shirikishi katika vituo vya kutolea huduma za Afya pamoja na kufanya vikao".Alisema.


Sambamba na hilo Afisa Lishe amebainisha kuwa  jumla ya wateja 264 waliohudhuria kliniki ya Baba ,Mama na mtoto katika hospitali ya Wilaya, vituo vya Afya na Zahanati wamepatiwa elimu.


Amebainisha kuwa katika kipindi cha robo ya Tatu, jumla ya watoto 2 waliogundulika na utapiamlo mkali wamepatiwa matibabu.


Sanjari na hayo, mhe Mussa Kilakala amewataka watendaji kata,Maafisa Tarafa pamoja na Maafisa kilimo, kuendelea na uhamasishaji wa utoaji wa chakula shuleni na kubainisha faida za wanafunzi kupata chakula shuleni na jinsi itakavyosaidia kupunguza utoro.

Aidha Halmashauri kupitia Sehemu ya huduma za lishe kwa kushirikiana na kitengo cha mawasilian o ya Serikali kimeendelea kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kufikisha Elimu ya Lishe kwa wananchi.




Tangazo

  • MPYA: TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA PANGANI May 10, 2023
  • MPYA: TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • MPYA: ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO September 09, 2023
  • MPYA: ORODHA YA WATAKAOENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO September 09, 2023
  • Angalia zote

Habari za Sasa

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI.

    May 23, 2025
  • WILAYA YA PANGANI YAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE – ROBO YA TATU 2024/2025.

    May 19, 2025
  • RC BATILDA AIPONGEZA PANGANI UANDIKISHAJI WA DAFTARI AWAMU YA KWANZA NA KUTOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA AWAMU YA PILI

    May 16, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI NA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI LAANZA PANGANI

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

ujenzi wa barabara ya Tanga pangani
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Mwongozo wa Tehama
  • Ratiba ya Vikao vya Halmashauri
  • Miongozo mbalimbali

Kurasa za mfanano

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Miongozo mbali mbali
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Pangani District Council

    Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga

    Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058

    Namba ya simu: 0658100588/062289307

    Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz

Mawasiliano Mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa