Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) ya Wilaya ya Pangani imewahamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sheria hiyo mpya inayolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya nchini.

Wito huo umetolewa leo, tarehe 10 Februari 2026, wakati wa kikao cha kamati hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri Mkoma.

Katika kikao hicho, wajumbe wa kamati walisisitiza umuhimu wa wananchi kuwa na bima ya afya ili kuhakikisha wanapata huduma za matibabu kwa urahisi na kwa gharama nafuu, pamoja na kupunguza mzigo wa gharama za matibabu kwa familia

Vilevile kamati imesisitiza umuhimu wa zoezi la umezeshaji wa dawa tiba kinga kwa watoto linarotajiwa kuanza hivi karibuni.
Aidha, ilielezwa kuwa gharama ya bima hiyo ni shilingi 150,000 kwa mwaka, ambapo itahusisha jumla ya watu sita (6) katika kaya moja.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa