Katika kuendeleza jitihada za kuimarisha ubora wa huduma za afya na kulinda usalama wa wagonjwa, tarehe 4 Februari 2026 Wizara ya Afya ilifanya tathmini ya nje ya utekelezaji wa afua za Kukinga na Kudhibiti Maambukizi (IPC) katika Hospitali ya Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga.

Tathmini hiyo ilitekelezwa kwa ushirikiano na shirika lisilo la kiserikali la CIHEB-Tanzania kupitia Mradi wa Usalama wa Afya Duniani.

Katika mchakato wa tathmini, shughuli za usimamizi elekezi pamoja na uwezeshaji wa watumishi katika vitengo mbalimbali zilifanyika, kwa lengo la kuimarisha uzingatiaji wa miongozo ya IPC na kuinua viwango vya usalama katika utoaji wa huduma za afya.
Hatua hizi zililenga pia kujenga uwezo wa watumishi na kuimarisha utendaji kazi wa kila siku katika mazingira ya hospitali.

Baada ya kukamilika kwa zoezi hilo, mrejesho wa matokeo uliwasilishwa kwa watumishi wa hospitali ili kuwezesha kuweka mikakati madhubuti ya maboresho, pamoja na kupanga hatua za ufuatiliaji na utekelezaji bora wa mapendekezo yaliyotolewa, kwa lengo la kuboresha zaidi ubora na usalama wa huduma kwa wananchi.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa