Na James K. Mwanamyoto, OWM TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewataka Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari, viongozi katika Sekretarieti za Mikoa na Serikali za Mitaa kutenga muda wa kusikiliza kero na malalamiko ya watumishi wa umma pamoja na wananchi kwa lugha ya staha.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo leo, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Wakuu wa Shule za Msingi uliohudhuriwa na Wenyeviti wa Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara, unafanyika katika Ukumbi wa Sephile Sapphire Pride uliopo jijini Dodoma.

“Tuwasikilize watumishi wenzetu pamoja na wananchi kwa lugha ya staha, tutachukua hatua ya kumuondoa yeyote atakayeshindwa kuwasikiliza watumishi na wananchi,” amesisitiza Prof. Shemdoe.
Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, suala hili la kuwasikiliza watumishi na wananchi lizingatiwe na Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na Wakuu wa Vitengo katika Halmashauri zote nchini ili waweze kutatua kero na changamoto zinazowakabili watumishi wa umma na wananchi katika maeneo yao ya kazi.
Pangani District Council
Sanduku la Posta: 89 Pangani -Tanga
Namba ya Mezani: +255 (0) 27 2630058
Namba ya simu: 0658100588/062289307
Barua Pepe : ded@panganidc.go.tz
Hakimiliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya Pangani .Haki Zote Zimehifadhiwa